RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

DR. FADHILI EMILY WA THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC AKISHIRIKIANA NA MADAKTARINI NCHINI ZIMBABWE WAKIFANYA UTAFIKITI WA TIBA NA MADAWA YA MAGONJWA MBALIMBALI


Kuna watu ambao Mungu amewepa karama fulani ya kusaidia jamii kwa njia fulani ambayo wewe huwezi kuifanya bila msaada wa Mungu. Dr. Fadhili Emily ni muumini wa kanisa la Wasabato. Kwa neema ya Mungu ameweza kutumia matunda na mimea kupata dawa mbali mbalimbali za magonjwa sugu yanayosumbua wanadamu duniani.

Dr. Fadhili Emily wa The Fadhaget Sanitarium Clinic kutoka Tanzania ambaye yuko nchini Zimbabwe kwa ziara ya maswala ya utafiti wa tiaba na madawa yake. Akiongea na Rumafrica kwa njia ya simu alisema, yuko nchini Zimbabwe kwa  lengo kubwa la kufanya utafiti juu ya vyanzo vya magonjwa  na matibabu yake.

Siku ya Jumamosi 23/08/2014 aliweza kufanikiwa kukaa na  vijana ambao ni madakatari wa Hospitali ya General ya Victoria Hills  iliyoko nchini Zimbabwe na kujua jinsi namna ya kuweza kuwasaidia wenye maradhi ya Tabia , Afya ya Uzazi pande zote yaani akina mama na akina baba na pia kuwatembelea wagonjwa katika wodi zao ili kuwafariji na kuwapa matumani kutokana na vile wanavyoteseka na magonjwa mbalimbali.

Dr Fadhili Emily aliweza kudokeza kile alichokiona na kujifunza pale tu alipoingia katika wodi ya akina mama ambapo aliweza kuona watu wawili tu kati ya mia moja ndio waliofanyiwa upasuaji, alizidi kusema, walipopewa takwimu ya juu ya wagonjwa wanatakiwa kufanyiwa upasuaji, ilionekana ya kwamba wagonjwa wengi (akina mama) hujifungua bila ya kufanyiwa upasuaji kwa sababu wana Elimu ya kutosha kuhusu afya ya uzazi. Kuna mambo mengi aliweza kuyafanya huko Zimbabwe ambayo si vyema kuyaongelea mitandaoni, ila unaweza kufika katika ofi zake na utajulishwa mengi juu ya tatizo lako la magonjwa.

Hayo ni baadhi ya mambo waliojionea huko Zimbabwe, hata kama tumekupa machache katika mengi ambayo Dr. Fadhili Emily aliweza kujionea na kujifunza, jinsi gani wenzaetu wa nchi za jirani wanapambana na magonjwa yanayowasibu.

Unaweza kufika katika makao makuu ya The Fadhaget Sanitarium Clinic ambayo yako Mbezi Beach Afrikana. Ukifika kituoni ulizazia watu wa bodaboda au bajaji wakuletea The Fadhaget.

Tunamuamini Mungu wetu kwa kila jambo. Mungu akubariki sana

MATUKIO KATIKA PICHA








 










Comments