RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

HATIMAYE DAWA YA EBOLA "ZIMAPP" YAONESHA MWANGA!



Tabasamu la matumaini baada ya kupata ahueni ya Ebola

Hospitali moja nchini Marekani imewaruhusu wamisionary wawili wa kimarekani ambao walikua wakipata tiba kutokana na kuathiriwa na virusi vya ugonjwa wa Ebola, na imethibitishwa hawana athari kwa afya ya
jamii. Dr Kent Brantly na mtabibu mwenziwe Nancy Writebol ambao waliruhusiwa mapema wiki hii walipata maambukizi ya ugonjwa huo wakati wakiwasaidia wagonjwa wa ugonjwa huo nchini Liberia.

Kutokana na maambukizi walopata watabibu hao walipata maambukizi walipewa dawa ya majaribio ambayo haikuwahi kupewa binadamu hapo kabla,na dokta aliyekuwa zamu alishindwa kuthibitisha juu ya nafuu yao kama imetokana na dawa hiyo ya majaribio.

Kufuatia matokeo mazuri ya dawa hiyo ya majaribio dokta huyo wa zamu alijinasibu kuwa kituo chake kimejifunza namna bora ya kumsaidia mgonjwa wa bola na mazingira alimokuwamo, na kuahidi kushirikisha utaalamu huo kwa watabibu kutoka katika nchi za Kiafrica

Comments