RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

IDADI YA WALIOKUFA KWA EBOLA YAFIKIA 1,350

Tuzidi kumuomba Mungu atuepushw na hili janga la ugonjwa wa Ebola. Ugonjwa huu unazidi kuteketeza watu, vifo vinaongezeka. Unapoomba maombi yako kumbuka kumuomba mweneyzi Mungu atusaidie kuondoa ugonjwa huu usije ukateketeza familia yako.

Mgonjwa wa Ebola akipelekwa eneo maalum kwa matibabu nchini Sierra Leone.

IDADI ya watu waliopoteza maisha kwa ugonjwa wa Ebola huko Afrika Magharibi mpaka sasa imefikia 1,350 kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Shirika la Afya Duniani (WHO) huku watu 106 wakiripotiwa kufariki kati ya Agosti 17-18 mwaka huu.

Ugonjwa huo ambao husambazwa moja kwa moja kupitia majimaji ya mwilini kutoka kwa mgonjwa mpaka sasa bado hauna tiba.

Source: Global Publisher

Comments