MATUKIO YA TAMASHA LA UZINDUZI WA ALBAMU YA IBRAHIM AHAZ SANGA NDANI YA LANDMARK HOTEL UBUNGO RIVERSIDE - DAR
Ibrahim Sanga kwa kupitia blogu hii anawashukuru watu wote waliofika katika tamasha lake lililofanyika hivi karibuni. Pia anamshukuru sana mgeni rasmi Mh. Mwigulu Nchemba, Mh. Martha Mlata Mbunge wa Singida, waimbaji wote na media zote na bila kusahau kampuni ya AGP Press kwa ushirikiano wao mkubwa kuhakikisha kazi ya Mungu inaenda kama ilivyopangwa. Mungu azidi kuwabariki katika kazi zenu na azidi kulinda afya zenu.
Ninaipongeza kamati yangu iliyoshiriki katika zoezi hili, hakika nimeona juhudi zenu na mafanikio makubwa ambayo sikutegemea kwa macho ya kibinadamu. Mungu atawalipa hapo mlipotoa.
Ninaipongeza kamati yangu iliyoshiriki katika zoezi hili, hakika nimeona juhudi zenu na mafanikio makubwa ambayo sikutegemea kwa macho ya kibinadamu. Mungu atawalipa hapo mlipotoa.
Ibrahim Sanga akisalimia na Mh. Mwingulu Nchemba
Ibrahi Sanga akiwa na stage show wake akimsifu Mungu wetu siku ya tamasha
Mh. Mwigulu Nchema akifungua rasmi DVD ndani ya kisanduku
Comments