SAFARI YA WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI TANZANIA CHINI YA CHAMA CHA MUZIKI WA INJILI TANZANIA WAKIELEKEA SINGIDA KUFANYA UMISHENI
SEHEMU YA TATU
Mwandishi na mpiga picha: Rumafrica.
Mwandishi na mpiga picha: Rumafrica.
Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa kuwatumia waimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania wakiongozwa na mlezi wa Chama hiki cha Muziki wa Injili Tanzania Mh. Martha Mlata kufanikisha safari hii kuwa ni ya salama na amani.
Rulea Sanga wa Rumafrica
Tukiwa safarini kuna mambo mengi tulikumbana nayo lakini Mungu alitutetea na kutuongoza salama. Tumeona ajali nyingi sana lakini sisi MUngu alituepusha na hayo yote. Tumekuwa tukimtukuza Mungu kwa uimbaji na kuomba tukiwa safarini na Mungu wetu aliweza kusikia maombi yetu na kutulinda.
Rulea Sanga
Dhumuni la waimbaji kufunga safari mpaka kijiji cha Ushora Kibaya , wilaya ya Iramba mkoani Singida ilikuwa ni kufanya umisheni, kuliombea Taifa la Tanzania amani na utulivu, kupanda miti kama moja ya utunzanji mazingira, kuhubiri Injili vijijini na kuwaleta watu kwa Bwana wetu Yesu Kristo pia kuonyesha mikanda au filamu za maisha ya Yesu Kristo iliwatu wajifunze na kuimarisha imani zao.
Rulea Sanga ndani ya Dodoma
Mji wa Dodoma
Kutoka kulia ni Pafii, Edson Mwasabwite, John Shaban, Rulea Sanga na Stella Joel
Kulia ni John Shabani na Rulea Sanga
Rulea Sanga
Edson Mwasabwite
Camera man Danny
Kulia ni camera man Danny na Pafii
Comments