RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

GLORIOUS WORSHIP TEAM INAKULETEA SUNDAY CELEBRATION

Hatimaye GWT kufanya tamasha lao la kwanza mwaka 2015 katika ukumbi tulivu wenye kiyoyozi wa Ginang Restaurant jengo la GEPF ulioko Victoria, barabara ya Bagamoyo mkabala na kituo cha mafuta cha Victoria jijini Dar es Salaam, na itakuwa siku ya Jumapili 22/03/2015 kwa kiingilio cha 10,000 tu.

Siku hiyo itakuwa ni siku ya pekee sana kwako wewe ambaye utafika eneo hilo kwaajili ya kumtukuza Mungu wetu kwa njia ya uimbaji. Kuna mambo mengi ambayo utafaidika siku hiyo ikiwa ni pamoja na kujiongezea imani yako katika kumtukuza Mungu na kumtengemea kwa kila jambo, na pia utaweza kukutana na watu mbalimbali ambao hujwahi kuwaona na ukapata muda wa kuchangia mawazo ya kimaisha.

Mungu atakwenda kuinuliwa siku hiyo kwa sauti zetu tukishirikiana na Glorious Worship Team. Waimbaji wengi watakuwepo siku hiyo kama uanavyowaona baadhi yao katika tangazo hapo juu. Tunaamini Mungu atakwenda kutubariki na kubariki kazi za mikono yetu siku hiyo.

Umefika wakati sasa wa walokole na watu wote wenye hofu ya Mungu kupenda kushabikia vitu vinavyofanywa na watumishi wa Mungu ili kuinua kazi ya Mungu. Shetani anafurahi sana anapokuona wewe unarudi nyuma katika kufanya kazi ya Mungu. Tunatakiwa kuwa na hasira ya kumuangamiza huyu shetani ili dunia nzima itawale uwepo wa Mungu na watu waishi kwa imani. Mtu wa kuwezesha kazi ya Mungu isonge mbele ni wewe na sio mtu mwingine.

TUONE BAADHI YA PICHA ZA GLORIOUS CELEBRATION WALIVYOWEZA KUTUMIKA KATIKA SEMINA YA KINABII YA NABII GODWIN WA GHANA MWAKA HUU
Hili ni eneo ambalo Glorious Worship Team wataweza kufanyia tamasha lao la Sunday Celebration.














Mungu awabariki sana watumishi wa Mungu, Tuonane siku hiyo.

Comments