RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

HARAKATI ZA UNCLE JIMMY: EDSON MWASABWITE ANUSURIKA KUCHOMWA KISU NA JAMBAZI KATIKA GARI LAKE



Ilikuwa siku ya alhamisi nilitoka nyumbani kwenda kariakoo kufika kariakoo nikakuta foleni….ilikuwa kubwa sana magari hayatembei unaganda sehemu moja kwa muda mrefu sana na hii ni kutokana na matengenezo ya barabara…. Nikiwa nimetulia sijui nitatoka vp ghafla nikamuona mtu mbele kushoto kwangu ananiambia rudi nyuma kidogo usije ukagonga daladala nikarudi nyuma.. Akanisogelea kwa dirishani na kuanza kuniambia tumekufuatilia sana tulitaka tukuibie… nilikuwa nimeshusha vioo kidogo hewa ingie akaniambia kwa vile unaonekana mtu unaemsikiliza kila mtu hatuwezi kukuibia ila usirudie kuacha vioo vya gari wazi, akajieleza kama mtu mwema kumbe bado ana nia ya kuniibia akaniambia nikuonyeshe mfano jinsi mtu anaweza kufungua mlango kioo kikiwa wazi akapenyesha mkono akatoa lok akafungua mlango wa gari huku nikiwa nimepigwa na butwaa nashangaa akaingia akakaa siti ya mbele akaniambia umeona nilivyoingia akaniambia naomba buku nikampa akaniomba elfu kumi nikamwambia sina akanitolea kisu akachukua pesa zote kwenye walet alikuwa anachukua kwa kutoa mifano namshukuru Mungu hakunidhuru aliniachia cm akashuka………….. Jamani wenye magari unaposimama na gari yako kwenye foleni funga vioo ni hatari kuacha vioo wazi bora uchome mafuta kuwasha kiyoyozi kuliko kuacha vioo wazi.

Comments