RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

BELLA KOMBO AAMUA KUOKOKA!



Mshiriki wa Bongo Star Search (BSS), mwaka 2010/2011, Bella Kombo.

Shani ramadhani

MSHIRIKI wa Bongo Star Search (BSS), mwaka 2010/2011, Bella Kombo ameweka wazi kuwa sasa hivi ameamua kumtumikia Mungu na kuachana na muziki wa kidunia aliokuwa akiufanya awali.

Akipiga stori na Amani, Bella alisema baada ya Shindano la BSS alikuwa anaimba katika bendi na pia ameshafanya kolabo na wasanii kama Hemed Phd, Tunda Man, Kala Jeremiah, Steve RnB, lakini mwaka jana aliamua kurudi rasmi kwenye nyimbo za Injili. “Nimekulia kwenye familia ya watu waliookoka kwa hiyo sijaanza kuokoka hivi karibuni ni malezi ambayo nimekuwa nayo tangu nimezaliwa na ninayaendeleza mpaka sasa, niko kwenye maandalizi ya kutoa albamu yangu ya nyimbo za Injili,” alisema Bella.

Comments