RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MCH. NOAH LUKUMAY AFUNDISHA JUU YA MTU WA NNE: KIPENGELE CHA PILI : MAOMBI YA KUKUTANA NA MTU WA NNE


Katika ibada ya “Kufunguliwa” iliyofanyika katika kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni “B” jijini Dar es Salaam kwa Bishop Dr. Gertrude Rwakatare, Mchungaji msaidizi wa kanisa hilo Mch. Noah Lukumay alifanya maombezi ya “Kukutana na Mtu wa nne” katika mihangaiko yako, na hivi ndivyo alivyoomba “Eeeh Bwana Yesu asante kwa siku ya leo kwani ninaenda kukutana na wewe kwa ishara na maajabu, jitukuze eeh Bwana kupitia Neno lako kwani Neno lako ni uzima, Neno lako ni afya katika mifupa yangu kwa Jina la Yesu, eeh Bwana Yesu Jumapili ya leo tunaiweka wakfu kwamba ni siku ya kukutana na mtu wanne katika maisha yetu kwa Jina la Yesu. 
Mzee wa kanisa

Eeh mtu wanne jitokeze katika maisha yangu, mahali nimeshindwa nisaidie, nisaidie, nisaidie kwa Jina la Yesu, kwa Jina la Yesu, kwa Jina la Yesu eeh Bwana Yesu asante kwa sababu wewe ni mwema kwa hao wakuchao, katika Jina la Yesu, amina. Baba MUNGU nasema asante kwa sababu ni majira ya kuzungumza na watu wako, ninashuka nisionekane MUNGU bali uonekane wewe, sauti yangu iwe moto, sauti iwe ni ngurumo na sauti yangu ikatende kazi yako, 

Bwana ukaitumie upendavyo katika Jina la Yesu mioyo ya watu wako ikagangwe, ikaponywe, kwa sababu wanakutumainia tu wewe, asante kwa siku ya leo, ninalibariki Jina lako tangu sasa na hata milele kwani unakwenda kujitukuza katika maisha yetu, ni katika Jina la Yesu Kristo, amina. Mwezi wa nne ninaenda kukutabna na mtu wa nne kwa Jina la Yesu, najua umejiandaa kukutana na mtu wa nne, iwe ni kwenye biashara yako kwa Jina la Yesu Kristo, 
iwe ni katika kazi yako kwa Jina la Yesu, natangaza iwe ni kwa watoto wako mtu wa nne kwa Jina la Yesu, natangaza huko kwa maboss awepo mtu wa nne kwa Jina la Yesu, popote unapoingia kuwepo na mtu wanne kwa Jina la Yesu, amina. 

Wazee wa kanisa




Comments