RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

PICHA 12 ZA VIWANJA 10 VYA NDEGE DUNIANI VILIVYOPITISHA ABIRIA WENGI ZAIDI 2015


Siku hizi kila kitu kina rekodi zake, kama wanatuambia mpaka idadi ya Tembo walioko Afrika hawawezi kushindwa kutuambia viwanja vya ndege vinavyoongoza kwa kupokea au kupitisha abiria wengi zaidi duniani.
NAMBA 10: Dallas Fort Worth uwanja upo Marekani na mwaka 2015 ulipitisha abiria milioni 64.

NAMBA 9: Paris Charles de Gaulle Airport Ufaransa ulipitisha abiria zaidi ya milioni 65

NAMBA 9: Paris Charles de Gaulle Airport kwa ndani Ufaransa ulipitisha abiria zaidi ya milioni 65

NAMBA 8: Hong Kong International ambao una sifa ya kupitisha tani kwa tani za mizigo, ulipitisha zaidi ya abiria milioni 68

NAMBA 7: Los Angeles International Airport Marekani, ulipitisha zaidi ya abiria milioni 74 mwaka 2015.

Las Angeles hiyo kwa ndani…

NAMBA 6: London Heathrow Airport ulipitisha zaidi ya abiria milioni 74.9

NAMBA 5: Tokyo Haneda Airport Japan na rekodi yake ni abiria milioni 75.

NAMBA 4: Chicago O’Hare International Airport Marekani

NAMBA 3: Uwanja wa ndege wa Dubai ambao ulishika namba 6 mwaka 2014 umezidi kusogea na kushika namba 3 mwaka 2015

NAMBA 2: BEIJING CAPITAL INTERNATIONAL AIRPORT CHINA ambapo abiria waliopita hapa mwaka 2015 ni milioni 89.9 na walitarajiwa kuwa wa kwanza mwaka 2015 sema hawajazifikia rekodi za uwanja namba 1

NAMBA 1: Uwanja wa Atlanta Hartsfield Jackson International ambao ulipitisha abiria milioni 100 kwa mwaka 2015 na kubaki namba 1 ileile ya mwaka 2014 kama Airport iliyokua busy kuliko zote duniani.

Comments