RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

HII NDIO KLABU YA KWANZA KUPANDA LIGI KUU UINGEREZA MSIMU UJAO 2016/2017



Wakati Ligi Kuu Uingereza ikiendelea kwa vilabu vya Tottenham Hotspurs na Leicester City kuchuana kwa karibu katika mbio za kuwania Ligi Kuu Uingereza, huku vilabu vya Newcastle United, Sunderland, Norwich City vikiwa katika hatua ya kupigania kutoshuka daraja na Aston Villa kuonesha dalili zote za kushuka, Bunley imekuwa klabu ya kwanza kurudi Ligi Kuu Uingereza msimu ujao.


Bunley wamefanikiwa kupanda Ligi Kuu Uingereza na watashiriki Ligi Kuu Uingereza msimu wa 2016/2017, nafasi hiyo wameipata baada ya kushinda kwa goli 1-0 dhidi yaQPR, Bunley wanarejea Ligi Kuu Uingereza wakiwa hawajafungwa mchezo wowote toka siku ya Boxing Day.