RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

KESI YA ASKOFU GWAJIMA 'WAKILI WA SERIKALI AGOMA KUPELEKA MASHAHIDI'.


Upande wa Mashitaka katika kesi ya Askofu Josephat Gwajima, Askafu wa Mkuu wa Kanisa la Ufufuo umekataa kuendelea kupeleka mashahidi wake katika Mahahaka yaHakimu Mkazi Kisutu kwa madai ya kutaka kesi isimamishwe ili isikilizwe rufaa yao.

Upande wa mashitaka ulipeleka mahakamani hapo notisi ya rufani tarehe 25 Aprilimwaka huu, kupinga kutopokelewa kwa ushahidi wao wa CD na picha zilizopelekwa mahakamani hapo.


Shadrack Kimaro, Mwanasheria Mwandamizi wa Serikali aliiomba mahakama kuwa, kesi hiyo isimamishwe mpaka utakapotolewa uamuzi wa rufaa ya kupinga kukataliwa kwa ushahdi wa CD na picha zilizofikishwa mahakamani hapo kama kielelezo cha kesi hiyo.

Shadrack amesema kuwa, ushahidi huo ulioambatana na ripoti ya mtaalamu wa picha na barua ya ZCO iliyokwenda kwa mtaalamu wa picha, vyote vilikataliwa mahakamani hapo.

Hata hivyo, upande wa mshtakiwa uliomba mahakama kufuta kesi hiyo kutokana na upande wa mashitaka kukosa ushahidi na kwamba kesi haiwezi kusimamishwa kutokana na kungojaa rufaa iliyokuwa bado haijafunguliwa.


Cyprian Mkeha, Hakimu Mfawidhi baada ya kusikiliza pande zote mbili amesema kuwa, kesi hiyo itatajwa tena tarehe 2 Juni mwaka huu.