Jumapili iliyopita ya May 22, 2015 lilifanyika Kongamano la Vijana lililoandaliwa na Huduma ya YOUTH FOR CHRIST MISSION(YCM). Kongamano hilo lilifanyika katika Kanisa la FPCT Magu-Mwanza na kuhudhuriwa na vijana toka madhehebu mbalimbali huku waimbaji mbalimbali pia walipata fursa ya kuhudumu katika Kongamano hilo.
Baadhi ya Waimbaji waliohudumu ni Adolph R. Nzwalla, Z. B toka Kenya, FPCT Magu Praise Team, pamoja na kwaya mbalimbali kama Bethania Choir na Vijana Amka Band.
Muhudumu wa Neno katika Kongamano hilo alikuwa ni Felista N. Emmanuel pamoja na Emmanuel Sowane. Hebu tazama namna mambo yalivyokuwa…..
Felista Emmanuel akiwa tayari kuhudumu kwa Neno
Baadhi ya Vijana wakiwa katika Kongamano
Z. B na Adolph Nzwalla wakihudumu
Vijana katika kongamano
Z. B na Adolph Nzwalla waki-perform
Vijana katika kongamano
Sifa ilipopamba moto
Z. B aki-perform
Vijana wakifuatilia jambo katika kongamano
Baadhi ya Waimbaji wa FPCT Magu Praise Team
Emmanuel Sowane, Felista Emmanuel na Adolph Nzwalla
Daniel, John na Dismas
YOUTH FOR CHRIST MISSION(YCM) ni Huduma inayojitegemea(isiyo chini ya dhehebu lolote) yenye lengo la kuhubiri injili kwa vijana ili wamjue Kristo na waishi maisha matakatifu kulingana na Neno la Mungu.
Source: Hossana Kwanza