RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MAMA AMBAYE ALIYEPOOZA AOMBEWA NA BISHOP DR. GETRUDE RWAKATARE NA KUWEZA KUTEMBEA



Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa matendo makuu anayofanya katika huduma ya Mlima wa Moto Mikocheni "B". Siku ya Jumapili 31.04.2016 Bishop Dr. Gertrude Rwakatare na jopo la wachungaji waliweza kumuomba muumini wa kanisa hili kwa tatizo lake la kupooza. Mungu aliweza kujibu maombi haya na mama huyu aliweza kutembea na kucheza muziki kidogo. Kama waamini tunasema Mungu ametenda na huo ulikuwa mwanzo. Unaweza ukawa na wewe umepooza lakini siku ya leo naomba ufike Mlima wa Moto Mikocheni "B" ukiamini kuwa unaenda kupokea muujiza wako. Imani yako inahitajika sana kwani imani yako yaweza kukuponya na kukuokoa.

Tunakuomba sana kama muumini na mtu mwenye upendo usikate tamaa kuwaombea hawa ndugu zetu wanaopitia magumu katika maisha yao. Leo kwao kesho hatujui itakuwa kwa nani. Tushikamane na tupebane wakati wa raha na shida