RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MASTER PROPHET DR. MACHBYA AHOFIA UKRISTO KUSHUKA CHINI

Kupitia Facebook akanti yake, Nabii Dkt. Machibwa alikuwa na haya ya kusema kuhusiana na Ukristo kushuka chini ukifananisha na Uislam duniani.

SHALOM WATUMISHI WA MUNGU.
Takwimu inaonyesha ulimwengu unawatu Billion 7, na katika hao wakristo hawafiki hata half yake, na mbaya zaidi uislamu ndio imani inayokua kwa kasi zaidi wakati Ukristo ukishuka.
Tukiangalia Tanzania peke yake kama case study, Tanzania ina watu wapatao Million 50, lakini watu waliookoka Tanzania ni Million 11 tu, maana yake watu Million 49 Bado hawajajisalimisha kwa Yesu. Hivyo basi tunakazi kubwa ya kufanya kupanga mikakati mipya ya kuifikisha Injili kwa wepesi na kuwafikia watu wengi zaidi kwaajili ya Kristo.
Badala ya kukaa kukosoana na kushambuliana, kupondana kwa lengo la kuharibiana, hebu kila mmoja ajipange kuipeleka injili kwa community yake.
Panga mikakati na tengeneza mazingira kwa kanisa lako ili wenye dhambi watamani kupata Mungu wako.
Mavuno ni mengi bali watendakazi ni wachache. Hebu tuamke na kuweka tofauti zetu kando na kuipeleka injili kwa nguvu. Kila mmoja akimuona mwenzake kuwa ni bora na kila mmoja akiutambua udhaifu wake. Mfano; Kama huna kifua cha kupiga mikutano ya nje, ukiandaa ita mwenzako unayejua amepewa neema eneo hilo tusaidiane. Kama huna uwezo wa kufundisha waongofu wapya usijikaze tafuta mtu mwenye neema eneo hilo. Hiyo ndio maana ya kupewa vipawa na karama na huduma kwa lengo la kufaidiana, ili mwili wa Kristo ujengwe na KAZI YA HUDUMA ITENDEKE.

Maana yake ni kwamba Tofauti zetu zisiathiri huduma na utendaji kazi, tuweke maneno kando tuifanye kazi yake yeye aliyetupeleka.
NAWAPENDA NA NINAWAHESHIMU WOTE.