RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

PICHA ZA GHOROFA (JUMBA JIPYA) LA ASKOFU DASTAN MABOYA.

(Picha ilipigwa na Rumafrica)

Ukifanya kazi kwa uamini naye Mungu atafanya kwako kwa uamini. Kazi ya Mungu mara nyingi huwa haendi bure. Ukiona wewe miaka nenda rudi unafanya kazi ya Mungu na hakuna mafanikio ujue kuna sehemu unakosea na una muudhi Mungu. Haiwezeka ukataabika kwa kazi ya Mungu halafu ukabaki kama alivyo. Mungu wetu ni Mungu anayebariki watu wake, na ndio maana hapa dunia kila mtu humpa riziki yake kutokana na juhudi zake za haki kujitafutia kile anachokitaka.

Leo hii tunamuona Askofu Mkuu Wa CAG, Mtume Danstan Haule Maboya. (huko mkoani Arusha)
ameweza kumpa nyumba nzuri, na huu ni ushuhuda mbele za watu kuwa Mungu wetu ni Mungu wa upendo na hujibu maombi yetu. Yaamkini Bishop Maboya alikuwa akiomba kila siku apate nyumba nzuri ili afanyike ushuhuda kwa waumini wake na wale wanaopenda huduma yake. Leo hii Mungu kamshangaza kwa nyumba nzuri. Tuzidi kumuombea akapate na nyingine nzuri zaidi kwa Jina lishindalo majina yote la Yesu Kristo.

Na wewe unayesoma gusa picha ya nyumba hii kwa imani ukapokee ya kwako kwa Jina la Yesu Kristo sema Amen.


Source Chief Hope