RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

RINGTONE ASEMA NYIMBO YAKE NA SHUSHO IMEMGHARIMU ZAIDI 21MILLION TSH



Alex Nyanchoga Apoko(Ringtone) ni mwanamuziki wa injili nchini Kenya ambaye amedumu Kwenye Industry kwa muda mrefu na amewahi kuonyesha nia ya kuwania ubunge katika jimbo moja nchini Humo.Hivi karibuni Ringtone amekuja na video ya nyimbo iitwayo TENDA WEMA ambayo amemshirikisha Christina Shusho.

Kwa mujibu wa Mtumishi huyo ambaye naye kama ilivyo kwa mwanamuziki mwingine wa nchini humo aitwaye Bahati, naye Ringtone aliwahi tangaza kuachana rasmi na muziki wa Injili nchini humo baada ya kuchoshwa na vitendo vya bifu baina ya wanamuziki wa injili wenyewe kwa wenyewe nchini humo sambamba na vuguvugu la wanamuziki wa injili kuamua kushushana kimuziki kwa makusudi.Akiongea na mtandao wa SDE Ringtone amesema nyimbo yake na Shusho imemgharimu 1Million Kenyan Sh ambayo kwa exchange rate ya leo 8.5.2016, 1Ksh=21.81Tshhivyo basi kibongo bongo Ringtone ametumia zaidi ya shilingi 21Million kwa video moja.

Uchukuaji wa video ukiendelea chini ya Director Tiger

Ringtone amezidi kusema sababu kubwa zilizopelekea video hiyo kufikia kiwango hicho ni pamoja na kukodisha ndege mbili(Chopa/Helicopter) zilizomgharimu kiasi cha Ksh 500,000/= sawa na zaidi ya 10M ya kitanzania pamoja na mambo mengine mengi alitumia zaidi ya 21M Tsh.Tukirudi nyumbani Tanzania gharama za Ringtone kufanya nyimbo moja kwa bei hiyo ni funzo tosha kwa Musicians wa Tanzania wanaotegemea chieap Video.

Video ya wimbo huo wa Tenda wema imefanywa imekuwa directed na award-winning videographerNelson Tiger wa Mind Vision kwa upande wa audio kazi hiyo imefanywa na producer Teddy B ambaye anaaminika nduo Top audio Producer kwa sasa nchini Kenya kwa upande wa Gospel.


Kazi Kazi