RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

BAHATI KUTOKA KENYA AWA MWANAMUZIKI WA KWANZA WA GOSPEL KUSHIRIKI KWENYE COKE STUDIO.

Hatimaye Bahati kutoka Kenya amepata nafasi ya kuchaguliwa kuingia kwenye Coke studio season 4 kwa mwaka huu wa 2016.Msimu wa nne wa Coke Studio umekuja wakati mwanamuziki huyo akiugulia machungu yakuwekwa kando kwenye tuzo za Muziki wa injili nchini Kenya(Groove Awards) zilizofikia kilele wiki mbili zilizopita.Hatua hii inamfanya Bahati kuwa mwanamuziki wa kwanza wa Gospel kuingia na kushiriki kwenye project hiyo toka ianzishwe,Bahati atakwenda sawa na wanamuziki wengine wakubwa na wakali kutoka sehemu mbalimbali za balani Afrika.

Bahati akiwa na moja kati ya Tuzo za Groove awards alizotwaa Mwaka jana 2015

Coke Studio Afrika ni Reality Tv Show inayodhaminiwa na kampuni ya Coca Cola ambapo wanamuziki na wasanii mbalimbali hikaa pamoja na kufanya mazoezi pamoja kasha wanakuwa na wasaa wa kuperfom on stage nyimbo zao na zile ambazo wanakuwa wamefanya kolabo ndani ya jumba hilo(Studio).Nchini Tanzania tumeshuhudia wanamuziki mbalimbali wakishiriki katika Coke studio Season ya kwanza mpaka ya tatu,wanamuziki hao ni pamoja na Diamond Platinum ,Joh Makini, Shaa, Vanessa Mdee, huku Fid Q na Ben Paul wao walishiriki msimu wa tatu wa Coke Studio uliomalizika miezi kadhaa iliyopita.

Kwa sasa Coke studio season 4 wanatarajia kuanza kushoot wiki ijayo ila kwa sasa maandalizi yanaendelea,nchini Tanzania Coke Studio Tv Show imekuwa ikionyeshwa na vituo mbalimbali vya Television nchini Ikiwemo ITV na Clouds Tv.