BISHOP DR. GERTRUDE RWAKATARE NA ASKOFU DANSTAN MABOYA WAZINDUA RASMI SEMINA YA CROSSOVER SIKU YA JUMAPILI 26.06.206 MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B"
Siku ya Jumapili ya 26.06.2016 Bishop Dr. Gertrude Rwakatare
alikuwa na ujumbe mzito katika ibada ya kufungua rasmi semina ya CROSSOVER
ambayo ilifunguliwa rasmi na Bishop Danstan Maboya. Semina hii inaendelea mpaka
Jumapili ya wiki hii hapa Mlima wa Moto kuanzia saa 9 mchana hadi usiku. Bishop
Dr. Gertrude Rwakatare alikuwa na haya ya kusema “Bwana Yesu Apewe Sifa!!.
Jamani Majaribu ni mengi, na majribu ni kama maji ya moto hayaunguzi nyumba na
katika jaribu kuna mlango wa kutokea. Hata mambo yakiwa mabaya acha kuzila
kanisa. Wengine wanafikiria kuwa Mungu wao amewaacha, nataka kukuambia kuwa
Mungu wako hajakuacha.
Ukisoma Nahumu 1:9 Neno la Mungu linasema, “Unawaza Nini Juu ya Bwana?” Katika
mapito yako unawaza nini juu ya Bwana? Bwana atakomesha majuto na misukosuko
yote. Kwahiyo ukijua kuna Bwana pembeni yako hata ukipita kwenye jaribu la
namna gani utapita tu. Ukisoma katika kitabu cha Kutoka 3:6-8, unatakiwa
kutafakari kama sisi ni wanadamu na tupo duniani na kwamba tunapatikana na
mamabya na tunapatikana na mema na tunapatikana na mazuri.
Unapomaliza nusu mwaka unatakiwa uwe na sababu ya kutafakari
uwepo wa Mungu katika maisha yako, lakini pia uwe na akili ya kuwaza kwamba
nusu mwaka nitaanzaje? Na ndio maana semina hii tumeweka ili tuweze kumkabidhi Mungu
ilia pate kuwa pamoja nasi ili yale mabaya ya nyuma yasitupate tena lakini mema
yaendelee kuimalika na yakupate kwa jina la Yesu.
Katika mwaka huu 2016 tumeanza na kishindo na vilio vya hapa
na pale, watu wengi wamekuwa wakilia, wengine wakilia na magonjwa, pesa,
biashara haziendi, kwa kweli kwa macho ya kwaida watu wana vilio hata kama watu
hawasemi, na wengine walikuwa na uwezo sana
zamani lakini leo wamekwama na wanatamani kuwa na Mungu. Wengine
wanadaiwa na ukiwadai wanasema, “Usiwe na wasiwasi tu nitakulipa”. Kwakweli
wapo watu wengine wamenasa
Nataka kuongea na Roho yako ya ndani ya mtu ambaye amenasa
na anashindwa kuendelea. Ulikuwa na maisha mazuri, lakini umejikuta uko mahali
unashindwa kuendelea na mahali ulipo hauna raha. Ile rajha ya mara ya kwanza
imepungua.
Sitaki uingie na uchungu nusu mwaka kuanzia Julai mpaka
Desemba 2016. Nataka uingie na furaha, nataka uingie na matumaini, nataka
uingie na Mungu, akushike kwa mkono wa
kuume wa haki Yake. Bwana Yesu apewe sifa.
Wako watu wamekwama na madeni, niangalie sana na sura za
huruma. Kama huna deni la benki basi unalo la SACCOSS au la PRIDE au la MPEMBA
nyumbani kwako. Ninaongea na wewe mwenye madeni ya kwamba fedha na dhahabu ni
mali ya Baba yako Mungu, hata kama una deoni kubwa la namna gani, Mungu anao
uwezo wa kukulipia, uwezo wa kukunansua. Nataka mwezi Julai usikufikia ukiwa na
masikitiko na machungu. Bwana anasema nimesikia kilio chako, nimeona madhaifu
yako.
Unajua kungekuwa na mahema ya kuweka nyumbani mwa kila mtu,
basi magari yasingepita, kwa maana kila nyumba kuna msiba, huzuni. Watu wengi wana mahema na wameweka mioyoni
mwao, na leo ni siku ya kularua mahema na matanga, mateso, huzuni, misukosuko.
Yaani ukifungua mioyo utatatua kukimbia
kutokana na machungu yaliyo ndani mwao.
Siku moja kulikuwa na mkutano wa akina mama Dodoma (WWA) na
mchungaji Maboya katika kanisa la Mch. Mhina, tukawa tumekusanyika tunaomba,
“Mungu tunataka tukuone, Mungu shuka” Mtu mmoja akasema nimemuona Malaika, watu
tukakimbia mbio. Ninaomba Mungu ajivunue kwako, Mungu ajivunue kwa matendo
makuu katika maisha yako.
Mama mmoja nyumba yake ilikuwa inauzwa kwani deni lake ni kubwa. Watu wakaanza
kusogelea katika ile nyumba ili wanunue. Mungu ataabisha maadui zako kwa jina
la Yesu, Mungu atafanya njia pasipo na njia kwa Jina la Yesu
Mch. Noah Lukumay (kushoto)