RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

BISHOP DR. GERTRUDE RWAKATARE NA ASKOFU DANSTAN MABOYA WAZINDUA RASMI SEMINA YA CROSSOVER SIKU YA JUMAPILI 26.06.206 MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B"



Siku ya Jumapili ya 26.06.2016 Bishop Dr. Gertrude Rwakatare alikuwa na ujumbe mzito katika ibada ya kufungua rasmi semina ya CROSSOVER ambayo ilifunguliwa rasmi na Bishop Danstan Maboya. Semina hii inaendelea mpaka Jumapili ya wiki hii hapa Mlima wa Moto kuanzia saa 9 mchana hadi usiku. Bishop Dr. Gertrude Rwakatare alikuwa na haya ya kusema “Bwana Yesu Apewe Sifa!!. Jamani Majaribu ni mengi, na majribu ni kama maji ya moto hayaunguzi nyumba na katika jaribu kuna mlango wa kutokea. Hata mambo yakiwa mabaya acha kuzila kanisa. Wengine wanafikiria kuwa Mungu wao amewaacha, nataka kukuambia kuwa Mungu wako hajakuacha.
Ukisoma Nahumu 1:9 Neno la Mungu linasema, “Unawaza Nini Juu ya Bwana?” Katika mapito yako unawaza nini juu ya Bwana? Bwana atakomesha majuto na misukosuko yote. Kwahiyo ukijua kuna Bwana pembeni yako hata ukipita kwenye jaribu la namna gani utapita tu. Ukisoma katika kitabu cha Kutoka 3:6-8, unatakiwa kutafakari kama sisi ni wanadamu na tupo duniani na kwamba tunapatikana na mamabya na tunapatikana na mema na tunapatikana na mazuri.
Unapomaliza nusu mwaka unatakiwa uwe na sababu ya kutafakari uwepo wa Mungu katika maisha yako, lakini pia uwe na akili ya kuwaza kwamba nusu mwaka nitaanzaje? Na ndio maana semina hii tumeweka ili tuweze kumkabidhi Mungu ilia pate kuwa pamoja nasi ili yale mabaya ya nyuma yasitupate tena lakini mema yaendelee kuimalika na yakupate kwa jina la Yesu.
Katika mwaka huu 2016 tumeanza na kishindo na vilio vya hapa na pale, watu wengi wamekuwa wakilia, wengine wakilia na magonjwa, pesa, biashara haziendi, kwa kweli kwa macho ya kwaida watu wana vilio hata kama watu hawasemi, na wengine walikuwa na uwezo sana  zamani lakini leo wamekwama na wanatamani kuwa na Mungu. Wengine wanadaiwa na ukiwadai wanasema, “Usiwe na wasiwasi tu nitakulipa”. Kwakweli wapo watu wengine wamenasa
Nataka kuongea na Roho yako ya ndani ya mtu ambaye amenasa na anashindwa kuendelea. Ulikuwa na maisha mazuri, lakini umejikuta uko mahali unashindwa kuendelea na mahali ulipo hauna raha. Ile rajha ya mara ya kwanza imepungua.
Sitaki uingie na uchungu nusu mwaka kuanzia Julai mpaka Desemba 2016. Nataka uingie na furaha, nataka uingie na matumaini, nataka uingie na Mungu, akushike kwa mkono  wa kuume wa haki Yake. Bwana Yesu apewe sifa.
Wako watu wamekwama na madeni, niangalie sana na sura za huruma. Kama huna deni la benki basi unalo la SACCOSS au la PRIDE au la MPEMBA nyumbani kwako. Ninaongea na wewe mwenye madeni ya kwamba fedha na dhahabu ni mali ya Baba yako Mungu, hata kama una deoni kubwa la namna gani, Mungu anao uwezo wa kukulipia, uwezo wa kukunansua. Nataka mwezi Julai usikufikia ukiwa na masikitiko na machungu. Bwana anasema nimesikia kilio chako, nimeona madhaifu yako.
Unajua kungekuwa na mahema ya kuweka nyumbani mwa kila mtu, basi magari yasingepita, kwa maana kila nyumba kuna msiba, huzuni.  Watu wengi wana mahema na wameweka mioyoni mwao, na leo ni siku ya kularua mahema na matanga, mateso, huzuni, misukosuko. Yaani ukifungua mioyo  utatatua kukimbia kutokana na machungu yaliyo ndani mwao.
Bishop Danstan Maboya


Siku moja kulikuwa na mkutano wa akina mama Dodoma (WWA) na mchungaji Maboya katika kanisa la Mch. Mhina, tukawa tumekusanyika tunaomba, “Mungu tunataka tukuone, Mungu shuka” Mtu mmoja akasema nimemuona Malaika, watu tukakimbia mbio. Ninaomba Mungu ajivunue kwako, Mungu ajivunue kwa matendo makuu katika maisha yako.
Mama mmoja nyumba yake ilikuwa inauzwa kwani deni lake ni kubwa. Watu wakaanza kusogelea katika ile nyumba ili wanunue. Mungu ataabisha maadui zako kwa jina la Yesu, Mungu atafanya njia pasipo na njia kwa Jina la Yesu
 




 
Mch. Noah Lukumay (kushoto)