RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

BISHOP DR. GERTRUDE RWAKATARE AMUOMBEA MCH. NOAH LUKUMAY SIKU YA JUMAPILI 19.06.2016 KATIKA KANISA LA MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B"

Baba katika jina la Yesu Kristo. Tupo mbele ya uso wako Mungu mwenye enzi, Mungu mkuu uliyetuumba na unayetulinda na kututetea. Asante Mungu uliyetuweka katika kanisa la Mlima wa Moto, ukatuosha kwa damu yako, ukatufanya ndugu wa Baba mmoja. Asante Mungu kwaajili ya kumuinua mchungaji wetu Noah Lukumay, tunakuomba Mungu kumtia nguvu pale anapojitoa, kwa kufunga, kwa kulia kwaajili ya kanisa lako. Mungu tunaomba umtie nguvu katika ujana wake. Tunavunja kila aina ya tamaa ya ujana, ikashindwe katika jina la Yesu, ukamvike utu uzima, mvike uzee katika jina la Yesu, tunamuomba adumu katika nyumba yako kwa Utukufu wa jina lako. Nalifunika kanisa zima ulilinde kwa jina la Baba na Mwana na Roho Mtaktaifu tumeomba..Amen