RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MFANYABIASHARA ALIYEKUWA AKIJIINGIZIA MILIONI 7 APANDISHWA TENA KIZIMBANI



Yusufali na mwenzake wakizungumza na mawakili wao, muda mfupi baada yakesi yaokuahirishwa.

Yusufali akishuka kizimbani.

Mfanyabiashara anayetuhumiwa kujiingia fedha zipatazo shilingi milioni saba kwa dakika, Mohamed Mustafa Yusufali amepandishwa tena katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu jijini Dar kusomewa mashtaka yanayomkabili.

Yusufali na wenzake, wanakabiliwa na mashtaka mbalimbali, yakiwemo udanganyifu, kughushi, kukweka kulipa kodi na kutakatisha fedha haramu pamoja na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya shilingi bilioni 15.6.

Hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo aliyefahamika kwa jina moja la Mashauri, ameiahirisha kesi hiyo mpaka Alhamisi ya Julai 28, 2016, baada ya upande wa mashtaka kudaiwa kuwa na upungufu katika hati ya mashtaka.

(Picha/ Habari: Hashim Aziz/ GPL)