RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

SIMU YA MH PAUL MAKONDA KWENYE CHOMOZA YA CLOUDS TV IMELETA HISIA NYINGINE.



Mh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ameguswa na Kipindi cha Gospel cha (CHOMOZA) kinacho rushwa na kituo cha Clouds TV na kupelekea kupiga simu Live na kueleza ni jinsi gani Kipindi cha Chomoza kimekua kikimbariki hasa kupitia watangazaji wake James Temu (Uncle Jimmy) na Samuel Sasali (Papaa).

Kati ya mambo aliyo eleza Mh Paul Makonda ni jinsi gani wema wa Mungu umekua mkubwa kwenye maisha yake. Ukweli ulio wazi Mungu amekua mwema kwangu, hapa nilipofika nakila sababu ya kushukuru wema wa Mungu kwani kuna mambo mengi amenivusha alisema Mh Mkuu wa Mkoa wa Dar Paul Makonda.