RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

PICHA 2: JACKLINE WOLPER KAONDOKA UKAWA… SASA HIVI NI CCM

Msanii wa filamu kutoka Bongo Movie Jackline Wolper jioni ya July 23 2016 akiwa katika mkutano mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mjini Dodoma alitangaza rasmi kurudi CCM, Jackline Wolper alitangaza kurudi CCM wakati wa mkutano huo ambao ulikuwa na kazi ya kumkabidhi uenyekiti wa chama Rais Magufuli.
Mwenyekiti mstaafu wa chama cha mapinduzi CCM akizungumza jambo na mwigizaji Jackline Wolper.

Kama utakuwa unakumbuka vizuri Jackline Wolper katika uchaguzi mkuu uliopita 2015, alikuwa akimuunga mkono mgombea urais wa CHADEMA Edward Lowassa ambaye alikuwa anaungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) ila kwa sasa ameamua kurudi CCM.


Picha zimetoka gazeti la Mwananchi.