RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

SONNIE BADU KUHUDUMU NAIROBI TAREHE ZILE ZILE AMBAZO UCHE ATAKUA DAR ES SALAAM

Mwanamuziki mahiri wa Injili barani barani Afrika Sonnie Badu ambaye anaaminika ndiye Mwanamuziki wa Kwanza wa Injili aliyefanikiwa Kifedha barani Afrika anatarajia kufanya huduma nchini Kenya katika kanisa la Jubelee Christian Centre linaloongozwa na Bishop Allan Kiuna na Mkewe Kathhy Kiuna.

Katika Kongamano hilo liitwalo DOUGHTERS OF ZIONI(Mabinti Sayuni) ni maalumu kwa mabinti na kwa muda sasa limekuwa Baraka kwa wengi huku mamia ya watu wakisafiri kutoka pande mabalimbvali za afrika kwa lengo la kujifunza kitu. Pastor Kathy Kiuna ndio mbeba maono wa Kongamano hili.


DOUGHTERS OF ZIONI inatarajia kufanyika tarehe 30/8/2016 mapaka tarehe 4/8/2016 nchini Kenya ambapo tarehe hizo hizo mwanamuziki nguli kutoka Joyous Celebration Ucheagu atakua nchini Tanzania jijini Dar es salaam akihudumu katika mkutano wa Injili uliopewa jina la Fire for Fire utakaofanyika viwanja vya chuo kikuu cha Dar es salaam. Kimsingi ujio was Sonnie Badu nchini Kenya ulianza kutangazwa mapema zaidi kuliko ujio wa Ucheagu nchini Tanzania.