RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

VIDEO: MTANZANIA ALIYETUNUKIWA TUZO YA HESHIMA YA VIONGOZI WA KESHO AUSTRIA, KAYAONGEA HAYA


Tanzania bado inaendelea kufanya vizuri kimataifa ambapo hivi karibuni iliingia kwenye headlines ya Mtanzania Seleman Kitenge kutunukiwa tuzo na Crans Forum vienna (Austria).

Seleman anaingia kwenye list ya kuwa mtanzania wa kwanza kutunukiwa tuzo hiyo zilizoanzishwa tangu mwaka 2010 ambapo atapata fursa ya kushiriki mikutano mbalimbali ya kimataifa.

Sasa Mtanzania huyu alikutana na Ayo TV na kueleza sababu zilizompelekea kutunukiwa tuzo hiyo ni kutokana na ushiriki wake wa mijadala mbalimbali ya kimaendeleo katika nchi za Russsia, Moroco na Azerbaijan, ndipo wadau wakapendekeza jina lake katika tuzo hizo pia ametoa wito kwa vijana wengine na kusema………

>>>‘Napenda kutoa wito kwa vijana wenzangu kuwa na uvumilivu na kuwa na moyo kujitolea katika programu mbalimbali za kulisaidia Taifa kama alivyosema katibu wa umoja wa mataifa kuwa hakuna jambo linatuhusu sisi bila sisi vijana’- Kitenge