RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

WANANDOA WAKIMSHUKURU MUNGU KWA KUWAFANIKISHA KATIKA HARUSI YAO MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B"

Hawa ni waamini wa kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B" ambao kwa neema ya Mungu waliweza kufunga ndoa yao katika kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B", na siku ya Jumapili 10.07.2016 waliweza kufika katika madhabahu ya Mlima wa Moto Mikocheni "B" na kumshukuru Mungu kwa sadaka kwa matendo makuu aliyoyafanya katika zoezi zima la harusi. Pia walimshukuru sana Bishop Dr. Gertrude Rwakatare kwa mchango wake na jinsi alivyowalea mpaka sasa wamekuwa mume na mke. Walimshukuru mchungaji wa maswala ya ndoa na Mchungaji kiongozi wa Mlima wa Moto Mch. Noah Lukumay kwa mafundisho yake na uvumilivu wake. Wanandoa hawa waliwashukuru wazee wa kanisa, vijana na kila mtu aliyehusika katika harusi yao. Alimaliza kwa kusema, "Mungu awabariki sana"