RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

WAZIRI MKUU UINGEREZA ACHAGUA MAWAZIRI WAPY


Waziri mkuu mpya wa Uingereza, Theresa May.

WAZIRI mkuu mpya wa Uingereza, Theresa May, ameanza kuchagua mawaziri wapya huku akiwaacha mawaziri waandamizi waliokuwa kwenye serikali ya David Cameron katika kile kinachoonekana anasafisha utawala uliopita na kuweka wake.

Vigogo waliotumbuliwa: Kutoka kushoto ni John Whittingdale aliyekuwa Utamaduni, Habari na Michezo; Nicky Morgan, aliyekuwa Elimu; Michael Gove wa Sheria na Oliver Letwin.

Mpaka sasa mawaziri wa zamani wanne wameondolewa kwenye nafasi zao ambao ni Michael Gove, Nicky Morgan, Oliver Letwin na John Whittingdale. Waziri mkuu huyo anataka kuwapa nafasi zaidi wanawake kwenye baraza lake jipya.

Mawaziri wapya walioteuliwa na May.

Mpaka sasa tayari amewateua Liz Truss (Waziri wa Makazi), Justine Greening (Elimu), Gavin Williamson (Sera na Bunge), pia anatarajiwa kuendelea ‘kutumbua majipu’ zaidi wakati