RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

APOSTLE SANJERI KUTOKA MAREKANI ASHANGAZWA NA KANISA LA MLIMA WA OTO MIKOCHENI "B" NA KUJIKUTA YUPO KANISA HAPO SIKU YA JUMAPILI 28/08/2016

APOSTLE  Sanjeri ambaye (Mkongo kwa asili) na mke wake (Mmarekani) kutoka Marekani siku ya Jumapili 28.08.2016 waliweza kuwasalimia waamini wa Mlima wa Moto Mikocheni “B”, alikuwa na haya ya kusema, “Tulikuwa na mkutano mahali lakini Mungu alitusimamia tukamaliza salama. Wakati tumefika hapa Tanzania tulikuwa tumefikia Hotel fulani hapa Dar es Salaam. Nilimpigia dereva wangu nikamwambia, “Bwana sijui kanisa la Mlima wa Moto liko wapi?”. Akasema, “Mimi ninapajua”. Namshukuru Mungu na leo hii nimeingia katika kanisa hili kwa mara ya kwanza na mke wangu ni mara yake ya kwanza kuja Tanzania. Nilipoingia mahali hapa nimesikia upako wa tofauti sana, nimesikia kitu tofauti ndani yangu, uwepo wa Mungu umetanda. Ninachotaka kusema ni kwamba kuna baadhi ya makanisa mengine hata Roho wa Mungu. Ninakuomba sana tuzidi kumtafuta Mungu kwa bidii.

 Kutoka kulia ni Aspostle Sanjeri, Mrs. Sanjeri na Bishop Dr Dr. Gertrude Rwakatare