RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

BISHOP GERTRUDE AFANYA MAOMBEZI SIKU YA JUMAPILI 31.2016 NDANI YA KANISA LA MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B"

Bishop Dr. Gertrude Rwakatare aliweza kufanya maombezi kwaajili ya kuvunja ngone za sheatani siku ya Jumapili 31.07.2016 katika ibada ya Tamasha la maombezi na Kuvunja Ngome za shetani lililofanyika katika kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni “B”, aliomba akisema, “Naomba sasa tuombe, sema, “Ewe magonjwa, ninakuamuru kwa jina la Yesu, toka katika maisha yangu na usirudi tena kwa jina la Yesu. Ewe matatizo ninakuamuru kwa jina la Yesu, ondoka katika maisha yangu, leo ni mwisho wako, mimi ninafunguliwa kwa jina la Yesu, toka katika maisha yangu katika Jina la Yesu Kristo. Ewe misukosuko, leo kwaheri kwa jina la Yesu, ondoka kwangu, ninakuamuru uniachie kwa jina la Yesu, toka kwangu na usirudi tena kwa jina la Yesu, ewe shida na mateso ninakuamuru utoke kwa jina la Yesu, Ewe Roho ya umaskini, ninakuamuru utoke kwa Jina la Yesu. Kuanzia leo Mungu wangu na Baba yangu ni tajiri, umeshindwa kwa jina la Yesu, napokea pesa kwa jina la Yesu na kuanzia sasa mimi nimefunguliwa katika jina la Yesu..Amen
 Mzee Mwakitalu (Mzee wa kanisa)