RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

DAVID ROBERT: SELF DETERMINATION NI MUHIMU SANA KUWA NAYO

Self determination kwa tafsili isiyo rasmi hiyari binafsi huu ni walaka wangu kwa rafiki zangu wote wa Facebook; Lipo jambo kubwa sanaa nimejifunza kuhusu kuhiyari binafsi. Kuna nyakati nyingi tunatengemea kampani katika kila tulifanyalo mfano maombi bila kundi la kuomba nao huombi, kufunga bila kanisa kutangaza program ya kufunga na kuomba hufungi, mazoezi wasipokuja mnaofanya nao hufanyi. Biashara mpaka usafiri na wengine ndio uende. Katika wokovu kwa sababu eti mchungaji kaanguka dhambini nawewe unaiacha imani. Hii ndio sababu kubwa sanaa wengi wamefeli.Mafanikio yeyote yawe ya ufaulu masomo,biashara,kiroho,afya,kumiliki na vingine kama hivyo, inahitaji jitihada binafsi (self determination) kwa kufuata wengine wanasema nini au watu wanalalamikaje juu ya hali ya uchumi huwezi kufanikiwa. Mimi Tumaini langu liko kwenye ahadi za Mungu na sio situation. Wote wanaweza kulalamika hakuna fedha lakini mimi Mungu wangu fedha na dhahabu ni mali yake. Waandishi wa vitabu vya uchumi wataandika utavisoma, wa vitabu vya ndoa utavisoma lakini bila self determination huwezi kufanikiwa. Mafanikio yako ndani yako zaidi fanya maamuzi sahihi. Badala ya kukaa vijueni au katika makundi ukiongelea watu fanya uamuzi wa busara hujachelewa. Hao unaowaongelea wenzako waliisha chukua hatua hayo unayoyatamani kwao yamo katika uwezo wako fanya uamuzi. Usizitumainie akili zako mtumaini Yesu yeye anaweza uwezi kuushinda uovu,dhambi,na uteka wako bila Roho mtakatifu. " ajapokuja huyo Roho wa kweli atawafundisha,atawakumbusha na kuwapasha habari za mambo yajayo. "ISN'T BEAUTIFUL TO HAVE JESUS" kama huna Yesu mtafute leo hii na utafanikiwa.