RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MAELFU WAPAKAWA MAFUTA YA UPAKO KATIKA KANISA LA MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B" SIKU YA JUMAPILI 21.08.2016

Mama wa Upendo Bishop Dr. Gertrude Rwakatare siku ya Jumapili 21.08.2016 katika ibada ya KUPIGANIWA NA MUNGU ambapo alifundisha juu ya NGUVU YA UPAKO katika kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B" aliweza kuwapaka mafuta ya upako waamini wa kanisa hilo na kila mtu aliyefika kuabudu siku hiyo.


Mafuta haya ya Upako ni mafuta yalioombewa na wachungaji wa kanisa hilo na kukabidhi kwa Mungu ili yakafanyike baraka katika maisha ya watu. Kupitia nguvu za Mungu zilizomo katika mafuta hayo yaliiombewa kwa Mungu, watu wakaweze kufunguliwa na Mungu katika vifungo vya mateso walivyofungwa kwa muda mrefu sana bila kufunguliwa. Mungu kupitia maombi ya mtumishi wake Mama wa Upendo Bishop Dr. Gertrude Rwakatare tunaamini ataweka mabo sana kwa watoto wake waliopakwa mafuta hayo na kuwekewa mikono na watumishi wake.

Tunakukaribisha na wewe ambaye hukubahatika kufika katika ibada hii ya tofauti kwa Jumapili hii. Itakuwa ni Jumapili ya kipekee katika maisha yao, ni siku ambayo itakuwa ni ya kihistoria maana Yesu Kristo mtenda miujiza atakwenda kukuondoa katika tope la manyanyaso ulimonaswa., katapila la Yesu litakunasua na kukuacha huru ukifurahia wokovu wako na maisha yako uyaliyobaki ya kuishi hapa duniani.

Ndugu yangu huu ni wakati wakp wa kujitakasa na kuishi maisha matakatifu ,aana hujui lililombele yako, kwahiyo heshimu sana sauti ya Mungu inayokujia kwa njia tofauti, yawezekana unapata ujumbe wa Mungu kwa njia ya mitandao, radio, TV, mikutano n.k, nakuomba sana heshimu na utii kama nafsi yako inataridhia kuwa ulichosoma na kusikia ni cha kweli.

Jumapili hii jitahidi kufika katika nyumba ya Bwana na ikiwezekana ukaona umefanya dhambi, kumbuka kutubu na kusinga mbele kumtumikia Mungu wako. Mungu wangu na akubariki sana. Ibada Jumapuli ni saa 9 mchana.