RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

TUCHEKI PICHA KADHAA ZA GODWIN MAIMU (NNYAKA) ALIVYOSHIRIKI KATIKA UZINDUZI WA DVD YA MESS JACCOB CHENGULA YA MOYO HAUNA WOGA


Godwin Maimu sio mtu wa kumuulizia sana, yeye ni mwimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania na hivi karibuni Mungu alimpa muujiza wa kupokea masters yake nchini Uingereza. Godwin Maimu ni moja ya waimbaji wanyenyekevu na wenye hofu ya Mungu na ni mwaminifu kwa kazi ya Bwana. Mwimbaji huyu amekuwa na neema ya pekee kutoka kwa mwenyezi Mungu kwani ameweza kufungua studio yake jijini Arusha inayoitwa God Win Nnyaka Production na pia Mungu amembariki na kazi nzuri katika benki ya CRDB hapa nchini Tanzania kama Meneja wa kanda ya kaskazini. Siku ya Jumapili 07.08.2016 aliweza kupata kibali mbele za Mungu na kushiriki tamsha la rafiki yake Mess Jacob Chengula lilolofanyika katika kanisa la Mito ya Baraka Kariakoo karibu na jengo la Yanga jijini Dar es Salaam. Tamasha hili lilihudhuriwa na waimbaji mashuhuri wa nyimbo za Injili Tanzania kama vile Goodluck Gozbert, Masanja Mkandamizaji, Upendo Nkone, Silase Mbise n.k.. Sasa tuone baadhi ya picha 
\