RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

DAVID ROBERT AMEACHIA UJUMBE MZITO SANA, JAMANI TUSOME

Katika vita ili umshinde adui lazima uwe na taarifa sahihi na za kutosha kumhusu. Ndio maana katika kila nchi kitengo cha intelijensia ni muhimu sanaa. Tanzania haiwezi kumpiga Malawi kirahisi mpaka tumepata taarifa muhimu kupitia maintelijensia wetu juu za uwezo wa adui kisiraha, idadi ya majeshi, umahili wa makamanda wa vikosi, mbinu zao za upiganaji na sehemu wanapohifadhi siraha.

Katika ulimwengu wa roho ni hivyo hivyo, kwanza lazima tukubaliane jambo la msingi kuwa vita yetu sio juu ya damu na nyama bali juu ya falme, pepo, sultan na majeshi ya kuzimu katika ulimwengu wa roho.

Katika tafakali nilikuwa naifanya leo Roho Mtakatifu amenipa taarifa za kiintelijensia juu ya adui yetu sitamtaja maana hana hadhi ya kutajwa kwenye post yangu yoyote ile, ila sote twamjua tena huyu sio adui tu ya waliokoka bali wote wenye mwili. Fuatana nami kwenye hii post utaelewa na utamchukia zaidi adui kama nimchukiavyo toka nilipopata ufunuo huu.

Siraha kubwa sanaa anayoitumia adui ni UMASKINI, herufi kubwa si kwamba nautukuza lah! Ila nataka hata mwenye matatizo ya macho aweze kuona na auchukie kwa nguvu zote na yeye alieuleta pia.

UMASKINI umekuwa chanzo cha migogoro katika ndoa, wote tunajua adui amewapiga zaidi wanaume kiuchumi maana anajua vema wao ndio providers wa familia. Angalia wakina baba wakishindwa kuprovide they die earlier kwa sukari, pressure, magonjwa ya moyo n.k. ukiangalia chanzo cha magonjwa hayo yoote ni msongo wa mawazo unaosababishwa na UMASKINI. Kumekuwa na tatizo kubwa kwa wanaume juu ya nguvu za kiume ukiangalia kiundani hakuna ugonjwa kama huo ni issue ya stress walizonazo juu ya maisha zinazowanyima hata hamu ya kushiriki vema tendo la ndoa.

UMASKINI umekuwa sababu ya dada zetu kuvuliwa nguo ili tu wapate ajira, fedha au favour ya jambo lolote wanaloitaji. Sio akina dada tu hata wanaume tumesaliti imani zetu kwa ajili ya fedha za rushwa au madili machafu.

Nimeyataja machache tu ambayo adui anashamulia kupitia siraha hii UMASKINI. Baada ya kupata taarifa hizi za kiintelijensia kutoka kwa Roho Mtakatifu nataka tuungane nawe rafiki kumpiga adui kwa nguvu zote ama kwa kufunga na kuomba uwe huru tu katika staili yoyote Roho atakayo kuongoza katika kuomba fanya.

Biblia inasema mpingeni adui nae atawakimbia.

MUNGU AKUBARIKI UNAPOUNGANA NA KATIKA KUMPIGA ADUI ILI ULIMWENGU UWE SALAMA.LOVE YOU LET'S NAIL HIM DOWN FOR THE GLORY OF GOD. HALLELUJAH