RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

PROFESA ANNA TIBAIJUKA KASHINDA TUZO NYINGINE MAREKANI



Usiku wa September 24 2016 heshima nyingine ya Tanzania iliandikwa nchini Marekani baada ya aliyewahi kuwa Waziri wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi Profesa Anna Tibaijuka kushinda tuzo ya kimataifa ya ‘His Royal Highness Prince Khalifa bin Salman Al Khalifa Award for Sustainable Development‘ ikiwa ni kutambua mchango wake katika kuhamasisha maendeleo duniani.

Tuzo hizi za heshima hutolewa kila baada ya miaka miwili ambapo washiriki wakuu huwa ni wale waliowahi kufanya kazi na shirika la umoja wa mataifa ambapo mwaka huu Waziri mkuu wa Bahrain Khalifa bin Salman ndiye aliyemkabidhi tuzo hiyo Profesa Tibaijuka.

Kazi ya utoaji wa tuzo hizi ulifanyika katika makao makuu ya umoja wa mataifa New York Marekani ambapo viongozi mbalimbali duniani walishiriki kushuhudia tukio hilo huku Tanzania ikisindikizwa na Waziri wa mambo ya nje Balozi Augustine Mahiga pamoja na mbunge wa viti maalum Anna Lupembe.

Unapoingia na kutoka katika ukumbi ulikuwa unakutana na picha hii

Profesa Tibaijuka na baadhi ya washiriki wakati wa utoaji tuzo

Profesa Tibaijuka akikabidhiwa tuzo hiyo ya heshima

Profesa Tibaijuka akitoa hotuba mbele ya waalikwa


Baadhi ya vyombo vya habari vya kimataifa viliripoti tukio hilo kama unavyoweza kujionea hapa kwenye hii video..