RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

SPIKA NDUGAI ATEMBELEA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR


Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai akiwasili Mjini Zanzibar kwa kutumia Boti wakati alipofanya ziara ya kutembelea Baraza la Wawakilishi mapema leo Septemba 2016.
Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai akisalimiana na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe Zuberi Ali Maulid (katikati) alipowasili katika Ofisi za Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Kushoto ni Naibu Spika wa Baraza hilo Mhe Mgeni Hassan Juma.
Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai (kulia) akizungumza na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe Zuberi Ali Maulid (katikati) na Naibu Spika wa Baraza hilo Mhe Mgeni Hassan Juma wakati alipowatembelea.
Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai (wa tatu toka kulia) akifuatilia kikao cha Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakati alipowatembelea. Wapili kulia ni Spika wa Baraza hilo Mhe Zuberi Ali Maulid na wa kwanza kulia ni Naibu Spika wa Baraza hilo Mhe Mgeni Hassan Juma.
Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai kiwasalimia Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar alipotambulishwa wakati wa kikao cha Baraza hilo.
Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe Zuberi Ali Maulid (kulia) na Naibu Spika wa Baraza hilo Mhe Mgeni Hassan Juma (kushoto).
Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe Zuberi Ali Maulid akimuelezea jambo Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai wakati wa ziara hiyo.