RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

25.09.2016: MCH. NOAH LUKUMAY: JI-CONNECT NA BISHOP DR. GETRUDE RWAKATARE UFANIKIWE KIROHO NA KIMWILI

Bwana Yesu asifiwe, ninachotaka kukuambia ni kwamba, Mungu anao uwezo wa kutenda mambo makubwa sana, ninakila sababau ya kumshukuru Bishop wangu mpendwa Dr. Gertrude Rwakatare yaani ninasema, “Mama mimi naogopa upako ulionao” . Bishop ana upako ndani yake, usioni sisi tulio chini yake tunachacharika na watu wanatokwa na mapepo na wengine wanabarikiwa, hapo ujue tunanyonya kutoka kwa Bishop Dr. Gertrude Rwakatare. 
Mch. Noah Lukumay 

Ukiona umekosa mahali pa kuchajia betri yako na mambo yako hayaendi kama ulivyopanga basi wewe ji-conect na Bishop Dr. Gertrude Rwakatare betri yako haitaisha chaji wakati wote, kila jambo ukilifanya linafanikiwa kwasababu Yesu yuko ndani yako kupitia watumishi wake. Tunaposema ku-jiconnect sio kujiunganisha na te 4G yenye MB nyingi ila tunamaanisha kwamba kuna huduma ndani yake Bishop Dr. Gertrude Rwakatare ambayo ukitaka kuambukizwa ni wewe kujiunganisha naye Kiroho. Mungu akubariki sana Bishop wetu kwa kuzidi kutulea na kutufanya tuwe na uzima. Miujiza yetu iko hapa, wewe usizanie mchungaji wako Noah Lukumay nimepokea mafanikio yangu nje ya nchi, nimepokea hapa hapa Mlima wa Moto Mikocheni “B”. Unaweza ukaambiwa maneno mengi sana wa watu nap engine kukatishwa tamaa lakini unatakiwa kujitambua uko sehemu gani kiimani na kujitambua wewe ni naåni.
åTunakukaribisha katika ibada ya Jumapili Mlima wa Moto Mikocheni "B" saa 3 asubuhi na siku ya Jumatano katika ibada ya KUFUNGULIWA KWAKO saa 9 mchana hadi usiku.