RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MAMBO YA KUFANYA ILI AFYA YAKO IKUWE MUZURI

NI NANI anayependa kugonjwa? Kwa kweli, ugonjwa unasumbua na unaomba feza. Wakati unagonjwa unajisikia mubaya, na pia hauwezi kuenda kwenye kazi ao kwenye masomo, hauwezi kupata feza, ao kuhangaikia familia yako. Unaweza hata kuwa na lazima ya mutu wa kukuchunga, na unaweza kulazimika kulipia dawa ao matunzo ya bei sana.

Ndiyo maana watu wanasema kuwa “Ni muzuri kuzuia ugonjwa kuliko kuuponyesha.” Kuna magonjwa fulani yenye hauwezi kuzuia. Lakini, kuna mambo mengi unaweza kufanya ili kuzuia ugonjwa usitokee mbio, ao hata usitokee. Ona mambo tano yenye unaweza kufanya leo ili ukuwe na afya ya muzuri.

1 UKUWE MUSAFI

Kulingana na hospitali moja ya Amerika inayoitwa Mayo, kunawa mikono ni “njia moja ya muzuri ya kuzuia magonjwa ao kufanya magonjwa yasiambukize watu wengi.” Njia moja ya mwepesi sana ya kupata mafua (grippe) ni kujigusa-gusa kwenye pua ao kwenye macho na mikono yenye kuwa na mikrobe ya ugonjwa huo. Namna ya muzuri ya kujikinga na ugonjwa huo ni kunawa mikono kila mara. Kuwa musafi kunaweza pia kuzuia magonjwa hatari sana, kama vile nimonia (pneumonie) na magonjwa ya kuhara. Kila mwaka, magonjwa hayo yanaua watoto zaidi ya milioni mbili wenye kuwa chini ya miaka tano. Tabia ya kunawa mikono kila mara inaweza hata kuzuia ugonjwa hatari sana wa Ebola usienee haraka.

Kuna wakati kunawa mikono ni jambo la lazima sana ili kulinda afya yako na afya ya watu wengine. Unapaswa kunawa mikono:

Kisha kutoka kwenye choo (W.C.).

Kisha kubadilisha nguo za ndani za mutoto (couches) ao kisha kumusaidia kutumikisha W.C.

Kisha kutunza kidonda.

Mbele na kisha kuwa pamoja na mugonjwa.

Mbele ya kupika chakula, kukitolea wengine, ao mbele ya kula.

Kisha kupiga chafya, kukohoa, ao kuondoa makamasi kwenye pua yako.

Kisha kugusa munyama ao mavi ya munyama.

Kisha kugusa uchafu.

Ni lazima kunawa mikono muzuri kabisa. Uchunguzi mbalimbali umeonyesha kuwa watu wengi hawanawe mikono ao hawanawe mikono muzuri kisha kutoka kwenye W.C. za watu wengi. Unapaswa kunawa mikono namna gani?

Ulowanishe mikono yako na maji yenye kuteremuka, kisha utie sabuni.

Usugue (usirite) mikono yako pamoja ili kutoa pofu, usisahau kusafisha makucha yote, nyuma ya mikono, na katikati ya vidole.

Uendelee kusugua mikono kwa segonde 20 hivi.

Usafishe mikono na maji safi yenye kuteremuka.

Ukaushe mikono yako kwa kutumia nguo safi ao karatasi ya kupangusa mikono.

Hayo ni mambo mepesi, lakini yanaweza kuzuia ugonjwa na kuokoa maisha.

2 UTUMIE MAJI SAFI

Katika inchi fulani, kupata maji safi kwa ajili ya familia yote ni kazi ya kila siku yenye kuchokesha. Mahali pa kushotea maji ya muzuri ya kunywa panaweza kuchafuliwa kwa sababu ya mvua nyingi, upepo mukali, ikiwa bomba (tuyau) la maji linavunjika, ao kwa sababu nyingine. Katika sehemu yoyote ya dunia, hilo linaweza kufanya ikuwe vigumu kupata maji safi. Kama maji hayatoke mahali safi ao hayachungwe muzuri, yanaweza kuleta magonjwa mengi, kama vile kolera, magonjwa ya kuhara yenye yanaweza kuhatarisha maisha, tifoide, magonjwa ya maini, na magonjwa mengine. Kila mwaka, inakadiriwa kuwa visa karibu miliare 1 na milioni mia saba vya magonjwa ya kuhara vinatokea kwa sababu ya kukunywa maji yasiyo safi.

Kuna mambo mengi unaweza kufanya ili kuzuia ugonjwa usitokee mbio, ao hata usitokee

Mara nyingi, mutu anapata ugonjwa wa kolera wakati anakunywa maji ao anakula chakula chenye kuwa na mikrobe yenye ilitoka katika mavi ya watu wenye kuwa na ugonjwa huo. Unaweza kufanya nini ili kujilinda na ugonjwa huo na magonjwa mengine yenye kuletwa na maji machafu, hata kisha tu musiba kutokea?

Ukuwe hakika kuwa maji yote unatumia juu ya kunywa, kusafisha meno, kufanya glase, kusafisha chakula na vyombo unatumia ili kula chakula, ao kupika, yanatoka mahali safi. Kwa mufano, unaweza kupata maji safi mahali pazuri penye watu wengi wanashotea maji ao utumie maji ya chupa zenye kufunikwa muzuri zenye kuuzishwa na shirika la maji lenye kuwa na sifa ya muzuri.

Ikiwa mahali unashotea maji pamechafuliwa, utokoteshe maji mbele ya kuyakunywa ao utumikishe dawa yenye kufaa ya kusafisha maji.

Wakati unatumia dawa za kusafisha maji, kama vile klorini ao vidonge (comprimés), ufuate kwa uangalifu maagizo ya mutengenezaji wa dawa hizo.

Utumie vyombo vizuri vya kuchuja maji, ikiwa vinapatikana na uko na uwezo wa kuvinunua.

Ikiwa dawa za kusafisha maji hazipatikane, unaweza kutia javel katika maji. Utumie tone mbili kwa litre moja, uchange muzuri, na kisha uache maji yatulie kwa dakika 30 mbele ya kuyatumikisha.

Uchunge maji yenye ulisafisha katika vyombo safi na vyenye kufunikwa muzuri ili yasichafuliwe tena.

Ukuwe hakika kuwa kila kitu kiko safi, kama vile kopo ao jagi yenye unatumia ili kushota maji.

Usafishe mikono muzuri mbele ya kugusa ao kubeba kitu chenye kuwa na maji ya kunywa, na usiingize mikono ao vidole ndani ya maji ya kunywa.

3 UKUWE MUANGALIFU NA CHAKULA UNAKULA


Haiwezekane kuwa na afya ya muzuri ikiwa mutu hakule muzuri, na ili kula muzuri uko na lazima ya chakula kizuri na cha aina mbalimbali. Ukuwe muangalifu ili usitumie chumvi nyingi, mafuta mengi, na sukari nyingi, na usikule sana. Ukule matunda na mboga za majani, na ubadilishe-badilishe chakula. Wakati unanunua mukate, chakula chenye kutengenezwa na mbegu, muchele, spageti ao makaroni, usome mambo yenye kuandikwa juu ya kitu cha kufungia ili ujue ikiwa vyakula hivyo vilitengenezwa na mbegu tu. Vyakula hivyo viko na nyuzi-nyuzi na vitu vya kujenga mwili kuliko hata vyakula vya namna hiyo vyenye vimechangwa na vitu vingine. Ili kupata proteini, ukule nyama ya kuku, na nyama zingine zenye hazina mafuta mengi, lakini usikule nyingi. Pia, ujikaze kula samaki mara nyingi katika juma, ikiwa inawezekana. Katika inchi fulani, inawezekana pia kupata proteini katika vyakula vyenye kutoka katika mimea.

Ikiwa unakula sukari nyingi na vyakula vyenye kuwa na mafuta mazito, unaweza kunenepa sana. Ili kupunguza hatari ya kunenepa sana, ukunywe maji kuliko kunywa vinywaji vya sukari-sukari. Ukule matunda mengi kuliko kula vyakula vitamu-vitamu kisha kula chakula. Usikule sana mafuta mazito yenye kuwa katika vyakula kama vile sosise, nyama, manteka (beurre), keki, jabini (fromage), na biskuti. Kuliko kutumia mafuta mazito ili kupika chakula, unaweza kutumia mafuta yenye kuwa muzuri zaidi kwa afya.

Chumvi nyingi ndani ya chakula inaweza kufanya damu itembee haraka sana katika mwili wako na kutia afya yako katika hatari. Ikiwa uko na tatizo hilo, usome habari zenye kuwa kwenye vitu vya kufungia chakula ili usitumie chumvi nyingi. Kuliko kutumia chumvi, utumie viungo vya kukoleza chakula na majani ya mimea fulani ili kufanya chakula chako kuwa kitamu.

Ni jambo la maana uchunguze ni chakula gani unakula lakini pia ni kiasi gani cha chakula unakula. Kwa hiyo, wakati unakula usiendelee kula ikiwa hausikie tena njaa.

Tatizo lingine ni kuwa chakula kinaweza kugeuka kuwa sumu. Chakula chochote kinaweza kuwa sumu kwa mwili wako ikiwa hakipikwe ao kuwekwa muzuri. Shirika la Afya Ulimwenguni (OMS) linaonyesha kama mamilioni ya watu wanagonjwa kila mwaka kwa sababu ya kula chakula kibaya. Wagonjwa wengi wanapona haraka, lakini wengine wanakufa. Unaweza kufanya nini ili kupunguza hatari hiyo?

Mboga za majani zinakomaa katika udongo wenye ulitiwa mboleo. Kwa hiyo, uzisafishe muzuri mbele ya kuzipika.

Mbele ya kupika kila kitu, unawe mikono, na usafishe kwa maji ya moto na sabuni vitu vya kukatia chakula, vyombo vya kupikia, vyombo unatumia ili kula, na meza za kuwekea chakula.

Ili chakula chako kisiambukizwe mikrobe na chakula kingine, uepuke kutia chakula mahali ao juu ya sahani yenye ilikuwa na mayai mabichi, nyama ya kuku ao nyama zingine bila kusafisha mahali hapo.

Upike chakula mupaka kiivye muzuri na usikawie kutia katika frigo chakula chenye kinaweza kuharibika haraka ikiwa hautakikula palepale.

Utupe vyakula vyenye vinaweza kuharibika vyenye vimefanya saa mbili ao moja katika chumba chenye kuwa na joto yenye kupita digri 32 za Selsiasi (32°C).

4 UFANYE MAZOEZI YA MWILI

Hata ukuwe na miaka ngapi, uko na lazima ya kufanya mazoezi ya mwili ili ukuwe na afya ya muzuri. Watu wengi leo hawafanye mazoezi yenye kuenea. Sababu gani mazoezi ya mwili ni ya lazima? Kufanya mazoezi ya mwili kunaweza kukusaidia:

Ulale muzuri.

Uendelee kuwa mwepesi.

Ukuwe na mifupa na mishipa yenye nguvu.

Usinenepe sana ao upunguze unene.

Upunguze hatari ya kupata ugonjwa wa kushuka moyo.

Upunguze hatari ya kufa haraka.

Ikiwa haufanye mazoezi ya mwili, unaweza:

Kupata ugonjwa wa moyo.

Kupata ugonjwa wa kisukari (diabète) wa aina ya 2.

Kupata tatizo la damu kutembea haraka sana katika mwili (hypertension).

Kuwa na kolesteroli nyingi katika damu.

Kupata ugonjwa wa kupooza.

Mazoezi yenye kukufaa yanategemea miaka yako na afya yako. Kwa hiyo, ni muzuri kumuona munganga mbele ya kuanza programu yoyote ya mazoezi. Mashauri mbalimbali yanaonyesha kuwa watoto wadogo wanapaswa kufanya mazoezi magumu na mazoezi mepesi kwa dakika 60 hivi kila siku. Watu wazima wanapaswa kufanya mazoezi mepesi kwa dakika 150 ao mazoezi magumu kwa dakika 75 kila juma.

Uchague mazoezi yenye kufurahisha. Unaweza kucheza basketi, tenisi, kabumbu, kutembea haraka, kutembeza kinga, kutunza bustani, kukata miti, kuogelea, kuendesha mutumbwi, kukimbia polepole, ao mazoezi mengine. Namna gani unaweza kujua ikiwa mazoezi fulani ni mepesi ao ni magumu? Jambo hili linaweza kukusaidia: mazoezi mepesi yanakufanya utoke jasho, lakini mazoezi mazito yanafanya ikuwe vigumu kwako kuzungumuza wakati unayafanya.

5 ULALE SAA ZA KUENEA

WATU wote hawana lazima ya saa zile zile za usingizi kwa siku. Watoto wengi wa chini ya mwaka moja wanalala saa 16 mupaka 18 kwa siku, watoto wa mwaka moja mupaka miaka tatu wanalala saa 14 hivi, na watoto wa miaka tatu mupaka ine wanalala saa 11 ao 12 hivi kwa siku. Kwa kawaida, watoto wenye miaka ya kuenda kwenye masomo wana lazima ya saa 10 za usingizi kwa siku, vijana wako na lazima ya saa 9 ao 10 hivi, na watu wazima wako na lazima ya saa 7 mupaka 8.

Ni jambo la lazima kabisa kulala saa za kuenea kila siku. Watu wenye elimu wanasema kama kulala saa za kuenea ni kwa maana sana ili kusaidia:

Watoto na vijana wakomae muzuri

Kujifunza habari mupya na kuiweka katika akili.

Mutu akuwe na kiasi kinachofaa cha homoni zenye zinasaidia ili chakula kitumike muzuri katika mwili, na kuwa na uzito wenye kufaa.

Moyo utumike muzuri.

Kuzuia magonjwa.

Inasemekana kuwa kukosa kulala saa za kuenea kunaleta tatizo la kunenepa sana, ugonjwa wa moyo, ugonjwa wa kisukari, na aksida. Kwa kweli, mambo hayo yanatuonyesha kuwa ni muzuri kulala saa za kuenea.

Kwa hiyo, unaweza kufanya nini ukiona kuwa uko na tatizo la kukosa kulala saa za kuenea?

Ujikaze kulala na kuamuka kwa saa ileile kila siku.

Ufanye chumba chako cha kulala kikuwe kimya, chenye giza, chenye kufurahisha, na kisikuwe na joto ao baridi nyingi.

Usiangalie televizyo ao kutumia vyombo vya kielektroniki unapokuwa mwenye kitanda.

Ufanye kitanda chako kikuwe kizuri, kulingana na uwezo wako.

Usikule chakula kizito na usikunywe kahawa, chai, ao pombe mbele ya kulala.


Ikiwa unatumia mashauri hayo lakini unaendelea kusumbuliwa na tatizo la kukosa usingizi ao matatizo mengine ya usingizi, kama vile kusinzia-sinzia muchana ao kushindwa kupumua muzuri wakati unalala, unaweza kumuona munganga mwenye kujua mambo hayo.

Ulinde Afya Yako

Afya yako inaweza kuharibika kwa sababu ya mambo fulani yenye hauwezi kuzuia, kama vile matatizo ya kupata feza, kukosa vitu vya lazima na mambo mengine. Hata hivyo, unaweza kujikaza kutumia mashauri fulani kati ya mashauri yenye kuonyeshwa katika habari yenye kutangulia. Kama vile mutu fulani mwenye hekima wa zamani alisema, ‘mutu mwerevu ni yule ambaye ameona musiba na kujificha.’—Methali 22:3.

Watu wenye kusoma Biblia wanafarijiwa na ahadi ya hakika yenye kuonyesha kama hivi karibuni, ‘hakuna mukaaji atakayesema: Mimi ni mugonjwa.’ (Isaya 33:24) * Mbele wakati huo ufike, ufanye yako yote ili kulinda afya yako na ya watu wenye unapenda.