RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

PAUL CLEMENT KUZINDUA VIDEO YAKE KWA ‘EXCLUSIVE PARTY’ LEO



Mwimbaji wa muziki wa Injili wa Kizazi kipya wa Tanzania Paul Clement siku ya leo Oktoba 7 anatarajia kufanya hafla maalumu ya uzinduzi wa video yake ya AMENIFANYIA AMANI katika Ukumbi wa LUTHER HOUSE uliopo mkabala na kanisa la KKKT AZANIA FRONT kuanzia saa 12 jioni ,hafla hiyo ikiwa imesimamiwa na uongozi wake wa FISHER RECORDs ambayo kwa sasa inasimamia kazi za msanii huyo.

Tanzania ikiwa inaongozwa na Paul Clement kuabudishwa kwa Upande wa Nigeria Nguli mwingine wa miondoko hiyo hiyo JOE PRAIZE yeye atawaabudisha Wanigeria siku hiyo hiyo na muda huo huo katika Uwanja mkubwa wa nchi hiyo uitwao TAKUBU GOWON STADIUM(FMR LIBERATION STADIUM)kuanzia saa 12 za jioni octoba 07 mwaka huu ambapo tukio hilo amelipa jina la TOTAL EXPERIENCE PORT HARCOUTY pia alimalizia kwa kusema haya baada ya mahojiano”There is NEW GLORY in this month OCTOBER Miracle are not needed in Heaven”

Joe Praize anatamba na wimbo wake mpya alioutoa mwaka huu ujulikanao kama Miracle Papa pia na nyimbo nyingi zilizo mtambulisha kama MIGHT GOD,UNCHANGEABLE,ALL PRAISE na kwa upande wa Paul Clement yeye anafahamika na nyimbo kama UMENIFANYA IBAADA,VITI HAVIFAI TENA.