RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

VIDEO: MBUNGE LEMA ALIVYOSIMAMA KUPINGA HOTUBA YA RC GAMBO


Leo October 18 2016 kumefanyika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika hospitali ya mama na mtoto inayojengwa eneo ya Burka nje kidogo ya jiji la Arusha, lakini shughuli hiyo ilisimama baada mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema kusimama kupinga hotuba iliyokuwa ikisomwa na mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.

Mbunge Lema alisimama kupinga hotuba hiyo akidai imejaa upotoshwaji na siasa ndani akisema yeye ndiye aliyetafuta eneo hilo la ujenzi kutoka kampuni ya Mawala Advocate na sio kweli eneo hilo limetokana na maono aliyokuwa nayo Marehemu Advocate Nyaga Mawala. Unaweza kuangalia video hii hapa chini.