RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

VIDEO:MERCY MASIKA – WAKENYA WAKO OPEN MINDED KWENYE FASHENI SIO KWAMBA HAWAJAOKOKA


Moja kati ya vitu vyenye utata kwenye tasnia ya muziki wa Injili ni namna ya uvaaji. Kuna tofauti kubwa ya uvaaji na muonekano kati ya waimbaji wa Kenya na Tanzania. Waimbaji wa Kenya wanaonekana kama hawako rohoni sana kutokana na namna yao ya kuvaa na jinsi wanavyoonekana mfano kuvaa hereni, kuweka dawa za ku breach kwenye nywele na vinginevyo.

GospoMedia ilipata nafasi ya kuongea na mwimbaji Mercy Masika kutoka Kenya ili kupata mtazamo wake wa tofauti ya mavazi na muonekano kati ya waimbaji wa Kenya na watanzania. Mercy amesema kuwa utofauti huo unatokana na tofauti ya tamaduni na pia ameeleza kuwa wakenya ni waelewa (open minded) kwenye masuala kama hayo ndio mana kwao kuvaa vipuli na kuweka breach sio tatizo.

Tazama zaidi kwenye mahojiano hapo juu. Kisha to maoni yako…