RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

HOJA YA HAJA: MATAMSHI MBALIMBALI YANAYOENDELEA HIVI SASA KATIKA SEKTA YA ELIMU; JE YANALENGA KUDUMISHA ELIMU AU YATABOMOA MISINGI IMARA YA SASA YA ELIMU?


Hivi karibuni kumetokea matamshi mbalimbali kuhusu mfumo mzima wa sasa wa elimu ya Tanzania; Baadhi ya hayo matamshi ni kitendo cha kutaka kubadili mfumo wa elimu kwamba eti kusomea degree ni lazima mwanafunzi awe amepitia kidato cha 6 pekee na si vinginevyo. 


Kwa Mataifa makubwa na yenye nguvu duniani kama Uingereza na mengineyo Mwanafunzi ana uhuru wa kusomea degree endapo kama anayo HND (Higher National Diploma) mfumo ambao ni sawa sawa na moja ya mfumo wa Sasa wa Tanzania ambao Mwanafunzi mwenye Diploma anaweza akasomea Degree.


Kwa mtazamo wangu endapo Mwanafunzi alishindwa kusomea Form 5 and 6 kutokana na Sababu zozote zile then baadae akaweza kujiendeleza kwa kusomea Cheti alafu Diploma ni sawa sawa na kumpatia a Second chance huyu Mwanafunzi aliyeshindwa kipindi cha nyuma; vile vile kumpatia Mwanafunzi huyu hii second chance kuna ongeza ongezeko la raia wenye elimu nchini Tanzania na kudumisha ustawi wa Taifa kwa kuwa na wananchi wengi wenye elimu na kufikia ndoto za kufanikikisha kuwa Taifa lenye Viwanda na human resource wenye competent skills.


Kutaka kuvunja mfumo wa Sasa sio jawabu pekee kwani Form 5 na 6 sio kitu cha ajabu; Cha msingi ni kuhakikikisha vyuo vinavyotoa certificates and diploma hivi sasa viwe na viwango vikubwa vya kutoa elimu iliyo bora ambayo inatakiwa. Kama mataifa makubwa kama Uingereza yenye elimu bora na kubwa duniani yanafuata mfumo wa HND (Higher National Diploma) then Degree; Je ni kwanini Tanzania ione mfumo huu ni mbaya??


Je kuleta haya mabadiliko ya haraka haraka kila kukicha bila ya kuwashirikisha wadau mbalimbali wa elimu na kushindwa kuongeza viwango vya elimu kwa kudumisha mfumo uliopo hivi sasa na kuongeza ubora wa elimu ya Tanzania ndio tuseme kutaongeza takwimu na ubora wa elimu nchini Tanzania??


Tukiwa tunabadili badili mifumo kila waziri mpya wa elimu anapobadilishwa au utawala unapobadilika je tunalipeleka wapi Taifa la Tanzania.


Elimu ya Tanzania ni swala muhimu na very sensitive na tukitaka Taifa la Tanzania kuwa kubwa duniani na lenye nguvu swala hili hasiachiwe mtu mmoja pekee kufanya maamuzi bali wadau wote kwenye sekta ya elimu na wananchi kwa ujumla washirikishwe.


Wadau wa elimu msikae kimya na kufumbia macho matamshi yanayoendelea na muweze kutoa maoni yenye kuendeleza elimu ya Tanzania kwa manufaa ya Watanzania na kwa Taifa hapo baadae.