RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MAADHIMISHO YA WIKI YA NENDA KWA USALAMA MKOANI MBEYA


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh.Amos Makalla akihutubia mamia ya wananchi katika sherehe ya maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama, Sherehe iliyo fanyika kimkoa katika Uwanja wa CCM Rwanda Nzovwe jiji la Mbeya. Sherehe hii iliyo wagusa wadau mbalimbali ikiwepo, Jeshi la Polisi, Wanafunzi, Mashirika ya kiserikali na Mashirika binafsi Pamoja na wananchi wote kwa ujumla katika jukumu la Kuzuia na Kupinga ajali za barabarani kwa kutii sheria Bila Shuruti.
Picha zote na Mr.Pengo wa Mmg Mbeya.

Bendi ya Magereza ikiongoza maandamano ya sherehe ya wiki ya nenda kwa usalama yaliyo anzia maeneo ya Soweto mpaka uwanjani Rwanda Nzovwe.


Baadhi ya madereva wa bodaboda wakiwa wamepozi kwa utulivu.
Mkuu wa mkoa wa Mbeya na mgeni rasmi wa sherehe ya maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama Mhe. Amos Makalla akipata picha ya pamoja na wadau wa Usalama Barabarani.