Siku ya Jumapili 30.10.2016 Bishop Dr. Gertrude Rwakatare,
Mch. Noah Lukumay, Mch. Francis Machichi, Mch. Elizabeth Lucas, Mch. Stanley
Nnko na wainjilisti wa kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni “B” waliweza kuongoza
ibada ya maombezi iliyokuwa inafanyika katika kanisa hilo.
Siku hiyo ilikuwa ni
tamasha la maombi la kihistoria. Watu wengi waliweza kufunguliwa na kupokea
miujiza yao, siku hiyo ilikuwa ni siku ya tofauti sana ukilinganisha na ibada
zingine zilizofanyika katika kanisa hilo kwa sababu kulikuwa na nguvu za Mungu
zilizo tanda kanisani hapo. Watu walitokwa na mapepo, majini, mikosi, laana n.k
kwa kupitia maombezi hayo.
Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa huruma zake
alizozifanya kwa kuwatumia watumishi wake katika ibada hiyo. Mungu ni Mungu wa
upendo kwani siku hiyo aliweza kugusa kila aliyefika katika kanisa hilo kwa
njia azijuazo yeye.
Pia tuna kila sababu ya kuwashukuru watumishi wa Mungu
walioweza kutii sauti ya Mungu na kuwahudumia watu wenye uhitaji waliofika
kanisani hapo wakiwa na mategemeo makubwa ya kupokea kile ambacho walikuwa
wanakitegemea kukipata kutoka kwa Mungu.
Tunakukaribisha wewe ambaye hukubahatika kushiriki ibada hii
ya tofauti siku ya Jumapili hii saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana. Jinsi ya
kufika kanisani ukifika kituo cha mabusi cha Makumbusho au Mwenge utakutana na
mabusi utasikia kwa Mama kwa mama hapo
yatakufikisha hadi kanisani wote mnakaribishwa sana.