RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MBUNGE JOHN HECHE ANUSURIKA KIFO KATIKA AJALI MOROGORO


Mbunge wa Tarime Vijijini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Heche leo amenusurika kifo baada ya gari alilokuwa anasafiria kutoka Dodoma kuelekea jijini Dar es Salaam kupata ajali eneo la Mikese mkoani Morogoro.


Chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika lakini kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo ni kwamba mbunge huyo amenusurika katika ajali hiyo na yupo salama.