RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

PICHA 20: BILIONI 215 ZILIVYOBADILISHA MUONEKANO WA JUMBA LA KIFAHARI LA DONALD TRUMP


Familia ya “Rais Mteule” wa Marekani Donald Trump inazidi kuzimiliki headlines kubwa wakati ikijiaandaa kuingia Ikulu ya White House. Mbali na nafasi aliyoipata mfanyabiashara huyo tajiri, Trump anaishi maisha ya kifahari kwenye jumba lake lenye thamani ya shilingi za Tanzania zaidi ya Bilioni 215.


Jumba hilo liko kwenye eneo lenye ukubwa futi za mraba elfu themanini (80,000) ufukweni mwa jiji la Florida. Trump alinunua jumba hilo kwa dola za Marekani Milioni 5 mwaka 1985 na kulifanyia ukarabati ambapo sasa lina vyumba vya kulala 58, bafu 33, jiko lenye meza za Marble kwa ukubwa wa futi 29, pamoja na sehemu za kuwasha moto 12.