RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

RAIS MAGUFULI ATENGUA UTEUZI MWINGINE LEO NA KUVUNJA BODI YA TRA

November 20, 2016 Nimepokea taarifa kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais IKULU Tanzania kuhusu Rais John Pombe Magufuli kutengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, Bernard Mchomvu kuanzia leo.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, Bernard Mchomvu.

Rais Magufuli amefanya utenguzi huo ikiwa ni pamoja na kuivunja Bodi yote ya Wakurugenzi huku taarifa ikisema kuwa uteuzi mwingine wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka hiyo utatangazwa baadaye.