RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

SIYO MAPENZI YA MUNGU WEWE UTESEKE!

Neno la Mungu linasema hivi:

"Je! Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini Mimi sitakusahau wewe. 
Tazama, nimekuchora katika vitanga vya mikono Yangu; kuta zako ziko mbele Zangu daima." - Isaya 49:15-16

Mwanadamu anaweza kukutenga, anaweza kukunyanyasa, anaweza kukufanyia mabaya; lakini USIKATE TAMAA. Haijarishi unapitia magumu kiasi gani: iwe katika ndoa yako, iwe katika biashara yako, iwe katika uchumba wako, iwe katika afya yako, iwe katika uchumi wako, iwe katika jamii yako, iwe katika masomo yako; USIKATE TAMAA, Jibu lipo, na ipo njia ya kutokea. Mwamini Yesu TAYARI amekushindia.

Hayo magumu unayapata ili imani yako izidi kukua hata Shetani apate kuaibika kwamba tayari ameshindwa tangu pale msalabani Yesu aliposema IMEKWISHA.

Pokea jibu la mahitaji yako sasa katika jina la Yesu Kristo. Amen.