RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

VIDEO: MAJIBU YA RC MAKONDA KUHUSU BARABARA KARIBU NA DARAJA LA NYERERE AMBAYO HAIJAKAMILIKA


November 20 2016 ni siku ya pili ya ziara ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda ambayo ameifanya kwa ajili ya kukutana na wananchi kwa ajili ya kujibu kero mbalimbali za wananchi, leo akiwa Kigamboni Dar es salaam amepita kwenye daraja la Nyerere ambapo mita chache kutoka daraja hilo kuna barabara ya takribani KM 1.5 ambayo haina Lami na ni mbovu.

Akizungumza na wananchi wa eneo hilo RC Makonda amesema barabara hiyo itaanza kujengwa baada ya wiki mbili……>>>’Nimeagiza ndani ya mwezi wa 12 barabara hii ianzwe kujengwa na tumeshakuvaliana ndani ya wiki mbili wataanza ujenzi’




VIDEO: Uchimbaji wa Kokoto ulivyoathiri eneo la Mji Mwema Kigamboni Dar es salaam