RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

07.12.2016: WAZEE WA KANISA WAPIGA PICHA YA PAMOJA SIKU YA JUMATANO YA SHILOH TANZANIA 2016 KATIKA KANISA LA MLIMA WA MOTO MIKOCHENI "B"

Wazee wa kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni "B" siku ya Jumatano 07.12.2016 katika kusanyiko la SHILOH ambalo hufanyika kanisani hapo mara moja kwa mwaka waliweza kupata picha ya pamoja kwaajili ya kumbukumbu. Shiloh Tanzania 2016 ambayo ilizinduliwa na Bishop Dr. Gertrude Rwakatare wa kanisa hilo akishirikina na Bishop Dunstan Maboya kutoka Arusha ilikuwa ni baraka kubwa sana kwa waumini wa kanisa hilo la Mlima wa Moto Mikocheni "B". Shiloh Tanzania itahitimishwa siku ya Jumapili 11.12.2016 kwahiyo ni vyema ukahudhuria kwa siku hizi chache ili upokee baraka za Mungu kutoka kwa Rev. Ndeda kutoka Afrika Kusini, Mch. Komba, Mch. Madoshi, Mch. Noah Lukumay, Mch. Karisto Kyando, Mch. Mama Mgetha, Mch. Elizabeth Lucas, Mch. Prisca, Mch. Simtomvu, Mch. Wambura, Mch. Dickson na wengine wengi ambao Mungu amewapaka mafuta kwaajili yako na mimi. Mungu akubariki, ibada yaShiloh itaanza saa 9 mchana hadi 12 jioni na kipindi cha maombezi kwa siku zote ni saa 4 asubuhi hadi 8 mchana.