RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

NABII RICHARD NA MKE WAKE NABII ANGEL RICHARD WASHEREKEA KRISMASI NCHINI MAREKANI

Nabii Richard Godwin wa huduma ya Jehovah Mercy Ministries na mke wake Nabii Angel Richard Krismasi ya 2016 waliweza kusherekea nchini Marekani katika ukumbi wa DMV. Nabii Richard alifanyika baraka sana kwa waliobahatika kufika eneo hili. Watu walipokea ujumbe aliouandaa kwaajili yao na pia kuwatabiria na kuwaombea. Ishara na miuijza iliweza kutokea kwasabau Mungu mwenyewee kupitia mtumishi wake aliweza kuwaponya wenye shida mbalimbali. 
Nabii Richard Godwin

Nabii Richard ambaye kwa sasa amefungua rasmi tawi la huduma yake Marekani amezidi kukonga mioyo ya Wamerekani na Watanzania waishio huko kwa mahubiri yake, na pia marafiki zake kupitia mitandao (social media) wamekuwa wakibarikiwa sana kutokana na comments tunazosoma katika post zake. Tunakila sababu ya kumuombea mtumishi wa Mungu asonge mbele katika huduma yake hii ya kinabii ili watu wapone mioyo yao na wamrudie Yesu Kristo.
Nabii Angel Richard
Sherehe ya Christmas yafana DMV

Prophet Richard Godwin